COSTECH Integrated Repository

Upande wa pili wa riwaya teule za Shafi Adam Shafi: dhamira zilizofichama

Show simple item record

dc.creator Haji, Gora Akida
dc.date 2019-08-28T09:24:16Z
dc.date 2019-08-28T09:24:16Z
dc.date 2015
dc.date.accessioned 2022-10-20T13:54:34Z
dc.date.available 2022-10-20T13:54:34Z
dc.identifier Haji, G. A. (2015). Upande wa pili wa riwaya teule za Shafi Adam Shafi: dhamira zilizofichama.Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/1203
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/1203
dc.description Tasnifu (MA Kiswahili)
dc.description Tasnifu hii ililenga kuchunguza Upande wa Pili wa Riwaya teule za Shafi Adam Shafi” kwa kuangalia dhamira zilizofichama. Utafiti uliofaywa uliongozwa na malengo matatu ambayo ni: Kuchunguza upande wa pili wa riwaya teule za Shafi A. Shafi kwa kuangalia dhamira zilizofichama katika kazi hizo; Kuchunguza na kubainisha miktadha mbalimbali iliyomsukuma Shafi A. Shafi kutumia mtindo huo katika kazi zake hizo; na Kubainisha athari za mtindo uliotumika katika kazi za Shafi A. Shafi kwa wasomaji wake. Mbinu zilizotumika katika ukusanyaji wa data ni udurusu wa maktaba, usaili na mahojiano ili kupata taarifa juu ya dhamira zilizofichama katika riwaya. Nadharia zilizotumika katika utafiti huu wakati wa ukusanyaji na uchambuzi wa data ni nadharia ya U-muundo na Umarx. Matokeo ya jumla ya utafiti huu yalionesha dhamira zilizofichama katika kazi teule kama zifuatazo: harakati za kupigania uhuru kuwa ngumu kutokana na vibaraka vya kikoloni kufaidika na utawala huo, ushiriki wa wasomi katika harakati za kupigania uhuru huo, kusalitiwa kwa wasomi baada ya kupatikana kwa uhuru huo pamoja na suala la ukweli kuhusu harakati za mapinduzi ya Zanzibar. Kutokana na matokeo haya, utafiti huu unashauri mambo yafuatayo: kwanza ni kuzisoma kazi hizi kwa makini ili kuweza kubaini kwa kina juu ya mambo yaliyofichama katika kazi hizi. Pili kazi hizi huweza kutumika kama rejea katika kuijua historia ya Zanzibar na Tanzania kwa jumla.
dc.language Kisw
dc.publisher Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.subject Riwaya
dc.subject Riwaya za Shafi Adam Shafi
dc.subject Shafi Adam Shafi
dc.subject Dhamira
dc.subject U-muundo
dc.subject Umarx
dc.subject Mitindo
dc.title Upande wa pili wa riwaya teule za Shafi Adam Shafi: dhamira zilizofichama
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
GORA AKIDA HAJI.pdf 910.2Kb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account