COSTECH Integrated Repository

Dhima ya tamathali za semi katika nyimbo za siasa za Wagogo

Show simple item record

dc.creator Mwakasaka, Kissa
dc.date 2019-08-29T11:41:26Z
dc.date 2019-08-29T11:41:26Z
dc.date 2015
dc.date.accessioned 2022-10-20T13:54:34Z
dc.date.available 2022-10-20T13:54:34Z
dc.identifier Mwakasaka, K., (2015). Dhima ya tamathali za semi katika nyimbo za siasa za Wagogo. Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma.
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/1298
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/1298
dc.description Tasnifu (MA Kiswahili)
dc.description Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kubaini dhima ya tamathali za semi katika nyimbo za siasa za Wagogo. Data zilikusanywa kutoka jamii ya kabila la Wagogo wanaoishi mkoa wa Dodoma, wilaya ya Kongwa kata ya Mtanana. Nyimbo mbalimbali za siasa zilikusanywa toka kwa wasanii mbalimbali wa kata ya Mtanana na kwa baadhi ya wananchi wa kata hiyo walihojiwa. Vilevile, zoezi la ushuhudiaji wa nyimbo za siasa ulifanywa na mtafiti. Aidha, mijadala mbalimbali ya vikundi ilifanywa. Nyimbo zilizokusanywa zilichambuliwa ili kuona jinsi tamathali za semi zinavyojitokeza, athari zake na dhima yake kwa jamii. Mbinu ya maelezo ilitumika katika kufanya utafiti huu na data zilichambuliwa kwa kutumia nadharia ya uhalisia wa kijamaa na nadharia ya U-Marx. Kadhalika, makala mbalimbali zilisomwa ili kupata data zinazohusiana na utafiti huu. Utafiti huu umebaini kuwa tamathali za semi zinazotumiwa na wasanii wa nyimbo za siasa toka katika jamii ya Wagogo hazitumiwi bure, bali zina dhima mahususi. Imebainika kuwa, tamathali za semi zinazojitokeza katika nyimbo za siasa za Wagogo zimejitokeza kwa namna mbalimbali zikiwa na dhima ya kuburudisha, kukosoa, kuokoa muda, kuhamasisha, kuweka msisitizo wa mambo, kuepusha migogoro, kuendeleza utamaduni na kujenga taswira. Utafiti huu ulibaini kuwa, wasanii wa nyimbo za siasa wamepevuka kisanaa kwani wanaweza kuweka vionjo vya kifasihi hasa katika matumizi ya lugha kwa kuweka tamathali za semi katika nyimbo zao kwa malengo maalum ambapo tamathali hizo za semi huleta athari mbalimbali kwa jamii.
dc.language Kisw
dc.publisher Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.subject Dhima
dc.subject Dhima ya tamathali
dc.subject Tamathali za semi
dc.subject Nyimbo
dc.subject Nyimbo za siasa
dc.subject Wagogo
dc.subject Nyimbo za Wagogo
dc.title Dhima ya tamathali za semi katika nyimbo za siasa za Wagogo
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
KISSA MWAKASAKA.pdf 989.1Kb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account