COSTECH Integrated Repository

Mdhihiriko wa mwendo katika ushairi wa kiswahili: Mifano kutoka katika diwani za wasakatonge na kimbunga

Show simple item record

dc.creator Mkombe, Vuai Pandu
dc.date 2021-01-26T07:01:43Z
dc.date 2021-01-26T07:01:43Z
dc.date 2020
dc.date.accessioned 2022-10-20T12:07:56Z
dc.date.available 2022-10-20T12:07:56Z
dc.identifier Mkombe, V. P. (2020). Mdhihiriko wa mwendo katika ushairi wa kiswahili: Mifano kutoka katika diwani za wasakatonge na kimbunga (Master's dissertation). The University of Dodoma, Dodoma.
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/2681
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/2681
dc.description Dissertation (MA Kiswahili literature)
dc.description Utafiti wa tasnifu hii ulichunguza mdhihiriko wa mwendo katika ushairi wa Kiswahili huku mifano ikitolewa katika diwani ya Wasakatonge na Kimbunga zilizotungwa na Mohammed S. Khatib na Gora Haji Gora. Mwendo katika ushairi wa Kiswahili ni kipengele cha kifani kinachotumiwa na watunzi kuboresha utunzi wa kazi za kifasihi na kudhihirisha ubingwa wa mtunzi katika kusana kazi zao. Hata hivyo, kipengele hiki cha mwedo hakijashughulikiwa sanakwa upande wa mashairi ukilinganisha na riwaya na tamthilia. Hivyo, mtafiti aliona ipo haja ya kukishughulikia.Kwa kiasi kikubwa, utafiti ulifanyika maktabani na uwandani. Data za uwandani zimepatikana kwa mahojiano ya sampuli iliyoteuliwa Data zilikusanywa katika mji wa Zanzibar. Mbinu ya maelezo ndiyo iliyotumika katika kutolea matokeo ya utafiti huu. Uchambuzi wa data umefanywa kwa kutumia nadharia ya upokezi kutokana na mihimili yake kufaa katika kubainisha aina, dhima na athari zake ukilinganisha na diwani teule na kufafanua miktadha mbalimbali inayohusiana na mwendo uliomo katika diwani hizo. Utafiti umebaini kuwa matokeo ya utafiti yanakwenda sambamba na malengo ya tasnifu hii kwa kuonesha usawiri wa vipengele vya mwendo, dhima na athari zake. Vipengele vilivyoibuliwa ni lugha, muundo, vina, wizani, maudhui, uteuzi wa maneno, mandhari na wakati, lafudhi, taswira, kibwagizo na maghani. Kwa upande wa dhima zilizojadiliwa ni pamoja na kutia hamasa za usomaji, kuibua hisia kwa wasomaji, kupendezesha mtu kusikiliza, kumpa uhuru mtunzi, kudhihirisha matumizi ya takriri, kujenga uwezo wa kufikiri, kuibua taharuki, chanzo cha kuibua maudhui, kuweka wazi nafasi ya mahadhi, kuonesha upekee wa mwandishi, mwendo kama kipengele cha kifani. Athari zimegawika katika sehemu mbili ambazo ni athari chanya zinazotokana na mwendo wa mashairi na athari na hasi. Athari chanya zilikuwa kama kufikisha ujumbe, kuleta uvuto kwa hadhira, kuleta msisimko, na kuchochea ukuaji wa lugha. Vile vile kwa upande wa athari hasi zilikuwa ni taaluma ndogo kwa hadhira, taaluma ndogo kwa waandishi, kuichosha hadhira na kupoteza taharuki. Mwisho mchango mkubwa wa utafiti huu ulibaini kuwepo kwa mwendo wa katika uga wa ashairi na hata katika ushairi wa Kiswahili.
dc.language Kisw
dc.publisher The University of Dodoma
dc.subject Ushairi
dc.subject Wasakatonge
dc.subject Kimbunga
dc.subject Mohammed S. Khatib
dc.subject Gora Haji Gora
dc.subject Kiswahili
dc.subject Mashairi
dc.subject Ukuaji wa lugha
dc.title Mdhihiriko wa mwendo katika ushairi wa kiswahili: Mifano kutoka katika diwani za wasakatonge na kimbunga
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
Pandu Mkombe Vuai.pdf 1.676Mb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account