COSTECH Integrated Repository

Taswira katika fungate ya Uhuru na Wasakatonge

Show simple item record

dc.creator Mkonda, Justine Jeremia
dc.date 2019-08-20T06:48:06Z
dc.date 2019-08-20T06:48:06Z
dc.date 2015
dc.date.accessioned 2022-10-20T13:54:34Z
dc.date.available 2022-10-20T13:54:34Z
dc.identifier Mkonda, J. J. (2015). Taswira katika fungate ya Uhuru na Wasakatonge. Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/976
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/976
dc.description Tasnifu (Shahada ya Uzamili Katika Fasihi ya Kiswahili)
dc.description Utafiti huu umehusisha taswira katika Fungate ya Uhuru na Wasakatonge. Chimbuko la tatizo limetokana na hali ya kila siku ya utumiaji na uelewaji mdogo wa taswira kwa wasomaji na wasikilizaji katika kazi mbalimbali za ushairi. Hivyo utafiti huu umejikita kuchunguza taswira katika diwani za Fungate ya Uhuru na Wasakatonge. Pia utafiti huu umekuwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni kuzichambua taswira zilizojitokeza katika diwani teule za mashairi ya Khatib, Aidha kuchunguza sababu za Khatib kutumia taswira katika diwani teule hizi na kubainisha matokeo ya matumizi ya taswira katika diwani za mashairi ya Khatib kwa wasomaji. Taarifa za utafiti huu zilikusanywa kwa njia ya mahojiano, majadiliano, madodoso na mapitio ya maandishi. Sampuli hizo zimegawa katika makundi mawili ambayo ni walimu wanao fundisha somo la Fasihi na wanafunzi wanaosoma somo hilo kwa kidato cha nne na kidato cha sita katika shule ya sekondari Ilolo na Vwawa. Uchunguzi wa taarifa za utafiti zilizokusanywa zimeongozwa na nadharia ya mwitikio wa msomaji ambapo uchambuzi ulifanyika kwa mbinu ya ufafanuzi. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kwamba diwani za Fungate ya Uhuru na Wasakatonge zina taswira nyingi ambazo zimejitokeza sehemu mbalimbali za diwani hizi. Taswira hizo zilizojitokeza ni zile za baadhi ya makundi ya kibayolojia, kiteolojia, na taswira za kawaida. Matokeo ya utafiti huu yamebainisha sababu mbalimbali za mwandishi Khatib kutumia taswira katika diwani teule. Sababu hizo ni pamoja na kuficha au kupunguza ukali wa maneno, kuwasilisha dhana moja kwa wakati mmoja na kuzileta hisia na fikra za wasomaji. Hata hivyo, utafiti huu umebainisha matokeo chanya na hasi ya matumizi ya taswira kama vile kupanua fikra za wasomaji na utata katika kupata maudhui yaliyokusudiwa. Mwisho utafiti huu umeonesha muhtasari wa utafiti, mapendekezo ya utafiti, matokeo ya utafiti, changamoto za utafiti na mambo mapya yaliojitokeza katika utafiti huu.
dc.language Kisw
dc.publisher Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.subject Taswira
dc.subject Fungate
dc.subject Uhuru
dc.subject Fungate ya uhuru
dc.subject Wasakatonge
dc.subject Ushairi
dc.title Taswira katika fungate ya Uhuru na Wasakatonge
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
JUSTINE JEREMIA MKONDA.pdf 2.483Mb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account