COSTECH Integrated Repository

Dhima ya nyimbo za bongo fleva zihusuzo rushwa katika kuleta mabadiliko kwa jamii

Show simple item record

dc.creator Sanga, Edomu Secondina
dc.date 2019-08-20T06:59:50Z
dc.date 2019-08-20T06:59:50Z
dc.date 2015
dc.date.accessioned 2022-10-20T13:54:34Z
dc.date.available 2022-10-20T13:54:34Z
dc.identifier Sanga, E. S., (2015). Dhima ya nyimbo za bongo fleva zihusuzo rushwa katika kuleta mabadiliko kwa jamii. Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/978
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/978
dc.description Tasnifu (shahada ya Uzamili ya Sayansi Jamii katika Fasihi ya Kiswahili)
dc.description Utafiti huu ulilenga katika kuchunguza Dhima ya Nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo Rushwa katika kuleta Mabadiliko kwa Jamii. Bongo Fleva ni nyimbo za kizazi kipya nchini Tanzania. Nyimbo hizi huwa na dhamira mbalimbali ambazo hulenga kuelimisha na kuburudisha jamii inayokusudiwa na msanii. Njia ya nyimbo huwa bora zaidi kwani huwafikia sehemu kubwa ya jamii. Kutokana na umuhimu wa nyimbo jamii hupata mwitikio na kuifanya jamii kupata mabadiliko na kuifanya jamii mpya yenye maadili mema. Nyimbo mara nyingi husadifu mazingira ya jamii anapoimbia msanii na zinalenga vyema katika kutambulisha utamaduni wetu kwa kuyaweka mambo yetu. Utafiti huu uliongozwa na malengo ya aina mbili ambayo ni lengo la jumla la utafiti ambalo lilikuwa kuchunguza dhima ya nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa kwa mabadiliko ya jamii. Pia malengo mahususi matatu, Kwanza kukusanya nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa zinazoimbwa na wasanii mbalimbali katika Jamii, Pili kuchunguza na kuainisha dhima zinazopatikana katika nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa, na Tatu kuchunguza mwitikio wa jamii kuhusiana na nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa. Utafiti huu katika nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa tulizozisikiliza na kuzitumia kama kifani chetu tulibaini dhima mbalimbali kama vile kuelimisha, kuarifu, kukemea, kuadili, kuonya, ukombozi, kudhihaki uoga, kutia hamasa, kupitisha amali za jamii na kutumika kama rekodi ya matukio muhimu katika jamii. Utafiti huu ulifanyika maktabani na uwandani, maeneo mbalimbali ya halmashauri ya jiji la Mbeya yalitumika katika kukusanya data. Nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa zilikusanywa na kuwekwa katika maandishi, kisha kuchambuliwa na kupata dhima zinazopatikana katika nyimbo kwa mabadiliko ya jamii. Mwitikio wa jamii kuhusiana na nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa na mwisho mabadiliko yaliyopatikana kutokana na nyimbo. Uchambuzi wa data umefanywa kwa kutumia mkabala wa U-marx, Matokeo yanaonesha U-marx unajikita katika kuleta mabadiliko kwa kujua historia ya jambo na kuelewa tatizo kisha kuliunda upya kwa namna bora zaidi tofauti na awali. Pia nyimbo za Bongo Fleva zihusuzo rushwa zimewekwa katika maandishi.
dc.language Kisw
dc.publisher Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.subject Nyimbo
dc.subject Nyimbo za bongo Fleva
dc.subject Rushwa
dc.subject Kizazi kipya
dc.subject Dhima ya fasihi
dc.subject Mbeya
dc.subject Tanzania
dc.title Dhima ya nyimbo za bongo fleva zihusuzo rushwa katika kuleta mabadiliko kwa jamii
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
EDOMU SECONDINA SANGA.doc.pdf 895.4Kb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account