COSTECH Integrated Repository

Athari za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa nyimbo za watoto waishio Mijini

Show simple item record

dc.creator Hemed, Bimkubwa Abdulrahman
dc.date 2019-08-20T08:29:34Z
dc.date 2019-08-20T08:29:34Z
dc.date 2015
dc.date.accessioned 2022-10-20T13:54:34Z
dc.date.available 2022-10-20T13:54:34Z
dc.identifier Hemed, B. A. (2015). Athari za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa nyimbo za watoto waishio Mijini. Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.identifier http://hdl.handle.net/20.500.12661/987
dc.identifier.uri http://hdl.handle.net/20.500.12661/987
dc.description Tasnifu ( Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili)
dc.description Utafiti huu umechunguza namna Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) inavyoathiri nyimbo za watoto hususan maeneo ya mijini ambako maendeleo hayo ya sayansi na teknolojia ndiko yanakopatikana kwa wingi. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Usosholojia iliyoasisiwa kwa kuja kupingana na ulimbwende karne ya kumi na tisa. Utafiti huu umejumuisha mbinu ya mahojiano na hojaji kukusanya data hatimaye imechanganuliwa kwa njia ya maelezo. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano yaliyopo nchini hususan mijini, yameathiri kwa kiasi kikubwa nyimbo za watoto kutokana na kuwepo kwa vyombo vingi vya habari hapa nchini, ambao ushindani wao wa kibiashara ndio unaowafanya warushe hewani nyimbo za wasanii mbali mbali na kuacha zile za watoto ambapo watoto walikuwa wanaziimba kabla yake. Suala la msingi lililobainishwa na utafiti huu ni kwamba nyimbo za watoto zimeathiriwa na maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano. Kutokana na matokeo ya utafiti huu, mapendekezo yafuatayo yamezingatiwa. Serikali na jamii wafanye juhudi za makusudi kurejesha hadhi ya nyimbo za watoto kwa kuziingiza katika mitaala ya shule pamoja na wazazi kufanya juhudi za makusudi kuwafundisha nyimbo hizo ili zisiendelee kupotea. Pia, imependekezwa tafiti zaidi zifanywe kuhusu tanzu mbalimbali za fasihi simulizi, na kwamba watafiti wasikidharau kipengele hiki cha nyimbo za watoto kwani mbali na kutoa burudani, pia watoto hupata mazoezi ya kutosha nakuwafanya wawe wakakamavu na wenye afya.
dc.language Kisw
dc.publisher Chuo Kikuu cha Dodoma
dc.subject Teknolojia ya habari na mawasiliano
dc.subject TEHAMA
dc.subject Nyimbo
dc.subject Nyimbo za watoto
dc.subject Mijini
dc.subject Usosholojia
dc.title Athari za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa nyimbo za watoto waishio Mijini
dc.type Dissertation


Files in this item

Files Size Format View
BIMKUBWA ABDULRAHMAN HEMED.pdf 1.375Mb application/pdf View/Open

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search COSTECH


Advanced Search

Browse

My Account