Utoshelevu wa Mawasiliano kwa Kiswahili katika Teknolojia ya Sikanu: Uchunguzi Kifani wa WhatsApp.

No Thumbnail Available

Date

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

University of Namibia

Abstract

Description

Abstract. Full text article available at http://journals.unam.edu.na/index.php/JULACE/article/view/1480
Makala hii inahusu uchunguzi wa utoshelevu wa mawasiliano kwa Kiswahili katika teknolojia ya SIKANU. Uchunguzi umejikita katika programu tumizi ya SIKANU ijulikanayo kwa jina la WhatsApp na simu ya mkononi aina ya Tecno F1 imetumiwa kama uchunguzi kifani. Utafiti umetumia mkabala wa kitaamuli, ambapo maelezo na maelekezo ya Kiswahili yaliyomo katika WhatsApp yamechunguzwa katika kupima utoshelevu wake. Vigezo vilivyotumika kupima utoshelevu wa mawasiliano hayo ni uelewekaji, uwepo wa msamiati katika kamusi za Kiswahili na katika matumizi ya wazungumzaji, ngeli za nomino, mpangilio wa viambishi na wa maneno katika tungo. Uchanganuzi umeonesha kuwa msamiati unaotumika katika WhatsApp, kwa kiasi kikubwa, ni toshelevu kiasi cha kukidhi mawasiliano baina ya watumiaji wake. Kuna msamiati ambao unafahamika na kuzoeleka kwa watumiaji na mwingine ni mapya. Msamiati mpya

Keywords

Teknolojia, KISANU, WhatsApp, Tecno F1., Swahili, Simu ya mkononi

Citation